SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL), limesema changamoto ya mrundikano wa madeni inaathiri utendaji wake na kusababisha lijiendeshe kwa hasraa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Hayo yamesemwa leo Ijumaa, tarehe 30 Julai 2021 na Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi, katika hafla ya kupokea ndege mpya aina ya Bombadier Dash 8-Q400, ya shirika hilo, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salam.
Matindi amesema kuwa, madeni hayo yanasababisha ATCL ishindwe kutanua mtandao wake wa safari za kikanda na kimataifa.
“ATCL ina changamoto ambazo zina athiri utendaji na kusababisha hasara, uwepo wa madeni yaliyorithiwa athari yake ni kushindwa kuongeza mtandao wa safari na kuongeza hasara ya uendeshaji kutokana na riba huchukuliwa kama gharama ya endeshaji,” amesema Matindi.
Matindi amesema kuwa, changamoto nyingine inayoathiri shirika hilo, ni muundo wake wa umiliki ambao kisheria huifanya kuwa mali ya Serikali.
“Muundo wa umiliki wa ndege ambao kisheria hufanya kuwa mali ya Serikali na hivyo kuhusisha na madeni ya Serikali. Athari ya muundo huo ni kushindwa kutekeleza utanuzi wa mtandao wa safari wa ATCL. Kutotanua mtandao wa safari kunaongeza hasara kwa Serikali kwani matumizi ya ndege yanaendelea kuwa ya chini,” amesema Matindi.
Akijibu malalamiko hayo, Rais Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake imezipokea na kwamba itazifanyia kazi.
“Kwa sababu ya muda nizungumzie kidogo masuala ya changamoto za shirika, kama mlivyomsikia mtendaji mkuu ametaja changamoto, niwaamabie kwamba changamoto zote tumezipokea na nataka nithibitishe kwamba, nimepokea mpango kazi wa shirika. Ofisi yangu itapitia kwa kushirikiana na shirika na wizara ili tuone inavyokwenda,” amesema Rais Samia.
TUONYESHENI MKATABA WA MANUNUZI YA NDEGE ,SI MLISEMA TUNAZINUNUA KWA PESA ZETU ZA NDANI (CASH) TUONYESHENI MKATABA AU HADI MAJI YAWAFIKE UTOSINI KAMA LILIVYOTUFIKA GONJWA LA KORONA NDIO TUKUBALIKUONYESHA MKATABA FEKI TUAMBIWE UKWELI YULE MKULIMA WA SOUTH AFRIKA ANATUDAI KIASI GANI NA DENI LA TAIFA NI KIASI GANI NA JE LILITOLANA NA NINI SABABU TULIAMINISHWA NA DIKTETA MAGU KWAMBA MIRADI YOTE PAMOJA NA NDEGE TUMENUNUANAKUIYENDELEZA KWA PESA ZETU ZA NDANI…