Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Aweso amng’oa bosi wa maji Sengerema
Habari Mchanganyiko

Waziri Aweso amng’oa bosi wa maji Sengerema

Juma Aweso, Waziri wa Maji
Spread the love

 

WAZIRI wa Maji nchini Tanzania, Jumaa Aweso, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, Mhandisi Robert Lupoja. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Aweso, amemteua Mhandisi Sadala Hamisi, kushika nafasi hiyo.

Taarifa iliyotolewa jana Jumatatu, tarehe 14 Juni 2021 na wizara hiyo imesema, Mhandisi Sadala kabla ya uteuzi huo, alikuwa mtumishi katika Wakala wa Majisafi na Mazingira Vijijini (RUWASA) DDCA.

Taarifa hiyo imesema, Awesso amefanya uteuzi huo kwa Mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa sheria Na 5 ya mwaka 2019 ambapo Mhandisi Robert Lupoja atapangiwa majukumu mengine.

“Katika hatua nyingine Waziri wa Maji amevunja bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Sengerema na taratibu nyingine za Kiofisi zinaende kufanyiwa kazi” imeeleza, taarifa hiyo.

Aweso, alichukua uamuzi huo, saa chache kupita tangu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kufanya ziara wilayani humo na kupokea kero mbalimbali ikiwemo ya maji.

Rais Samia, alionyesha kukerwa na kitendo cha mamlaka ya maji, kudaiwa fedha na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akisema “sasa kama wananchi wanalipa bili ya maji, kwa nini fedha hizo hazitumiki kulipa Tanesco.”

Kutokana na hatua hiyo, Rais Samia alisema, kuna jambo la kufanya wialayani Sengerema kwani kuna mambo hayaendi sawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!