Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Balozi aliyeuawa Congo, mwili warejeshwa Roma
Kimataifa

Balozi aliyeuawa Congo, mwili warejeshwa Roma

Spread the love

 

MWILI wa Luca Attanasio, aliyekuwa Balozi wa Italia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), umerejeshwa Roma nchini humo kwa ajili ya maziko. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Kundi la waasi, DRC lilivamia na kushambulia magari ya Umoja wa Mataifa (UN), ambapo kwenye msafara huo, alikuwemo balozi huo.

Tukio hilo lililosababisha kifo cha Attanasio, mlizi wake Vittorio Lacovacci na dereva wake, raia wa DRC aliyetajwa kwa jina la Moustapha Milambo, lilitokea juzi Jumatatu tarehe 22 Februari 2021.

Magari hayo ya UN, yanaelezwa kwamba yalikuwa yamebeba chakula cha msaada. Mashambulizi hayo yalitokea Goma, mashariki mwa nchi hiyo.

Waasi hao walipanga kuteka nyara magari hayo na mali zote, hata hivyo hawakufanikiwa.

Mwili wa balozi huyo sambamba na wa mlinzi wake, ulisafirishwa kwa ndege ya Jeshi la Italia.

Miili hiyo iliokuwa imefunikwa kwa kitambaa cha bendera ya taifa hilo, ilipokewa katika Uwanja wa Ndege wa Ciampino na Waziri Mkuu, Mario Draghi.

Serikali ya DRC, imeelekeza tuhuma na lawama zake kwa kundi la waasi wa Rwanda, FDLR kwamba ndio lililohusika kwenye mauaji hayo. Hata hivyo, FDLR limekanusha kuhusika na shambulio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!