MWILI wa Luca Attanasio, aliyekuwa Balozi wa Italia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), umerejeshwa Roma nchini humo kwa ajili ya maziko. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).
Kundi la waasi, DRC lilivamia na kushambulia magari ya Umoja wa Mataifa (UN), ambapo kwenye msafara huo, alikuwemo balozi huo.
Tukio hilo lililosababisha kifo cha Attanasio, mlizi wake Vittorio Lacovacci na dereva wake, raia wa DRC aliyetajwa kwa jina la Moustapha Milambo, lilitokea juzi Jumatatu tarehe 22 Februari 2021.
Magari hayo ya UN, yanaelezwa kwamba yalikuwa yamebeba chakula cha msaada. Mashambulizi hayo yalitokea Goma, mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi hao walipanga kuteka nyara magari hayo na mali zote, hata hivyo hawakufanikiwa.
Mwili wa balozi huyo sambamba na wa mlinzi wake, ulisafirishwa kwa ndege ya Jeshi la Italia.
Miili hiyo iliokuwa imefunikwa kwa kitambaa cha bendera ya taifa hilo, ilipokewa katika Uwanja wa Ndege wa Ciampino na Waziri Mkuu, Mario Draghi.
Serikali ya DRC, imeelekeza tuhuma na lawama zake kwa kundi la waasi wa Rwanda, FDLR kwamba ndio lililohusika kwenye mauaji hayo. Hata hivyo, FDLR limekanusha kuhusika na shambulio hilo.
Leave a comment