Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli akumbusha machungu ya Waziri Mkuu Pinda
Habari za Siasa

Magufuli akumbusha machungu ya Waziri Mkuu Pinda

Hayati John Magufuli
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amekumbusha ‘machungu’ ya Mizengo Pinda, aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya awamu ya nne kuhusu bomoabomoa ya Jengo la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amekumbushia mvutano huo akisema, alipokuwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, alitaka kuvunja sehemu ya jengo hilo iliyojengwa katika hifadhi ya barabara, ili kupisha ujenzi wa barabara lakini Waziri Mkuu, Pinda alimpinga.

Rais Magufuli amesema hayo wakati akizungumza katika uzinduzi wa Daraja la Juu la Kijazi, Ubungo Dar es Salaam leo Jumatano tarehe 24 Februari 2021.

Amesema, baada ya kuingia madarakani, aliamua kufuata sheria kwa kulivunja jengo hilo, kisha kuanza ujenzi wa barabara ikiwemo daraja hilo.

“Namkumbuka mtani wangu Pinda akiwa waziri mkuu wakati huo, akaniambia kweli mtu anaweza akaenda kuvunja jengo la Tanesco? Sasa mwambie Pinda jengo la Tanesco tumelivunja, tuko hapa,” amesema Rais Magufuli.

Amesema, alichukua hatua hiyo ili kukidhi matakwa ya sheria dhidi ya watu waliokiuka sheria kwa kujenga ndani ya hifadhi ya barabara.

“Mtanishangaa huyu anamsema aliyekuwa waziri mkuu wake, ndio sababu sheria ni msumeno, nawaomba watendaji wasimamie sheria.”

“Haiwezekani ukaenda kubomolesha watu Kimara, ukawaacha waliovunja sheria, wengine walio ndani ya serikali, tutakuwa tunawaonea wananchi,” amesema Rais Magufuli.

Mizengo Pinda

Mbali na kukumbushia ‘mvutano’ wake na Pinda, amesema, kuna baadhi ya watu ndani ya serikali walimshangaa kufuatia hatua yake ya kubomoa yaliyokuwa majengo ya Ofisi ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mkoa wa Dar es Salaam.

“Hapa tulipokaa, ilikuwa ndiyo Makao Makuu ya Tanroad Dar es Salaam, kama yupo hapa Mhandisi Ndiyamkama ilikuwa ofisi yake nikaja nikabomoa, walinishangaa kweli hata ndani ya serikali walinishangaa,” amesema Rais Magufuli.

Amesema, hatua yake imefanikisha ujenzi wa barabara na daraja hilo “lakini ni kweli, sisi serikali hatuwezi kuongoza kwenye kuvunja sheria, sheria ni msumeno. Leo pamependeza, jengo hili nilisema hiki kipande cha Tanesco kiko ndani ya barabara.

1 Comment

  • Big up our president.Njoo kasulu vijijini uone kero za migogoro ya ardhi.wananchi tunateseka huku. thanks

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!