Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gari la Bobi Wine lashambuliwa kwa risasi
Kimataifa

Gari la Bobi Wine lashambuliwa kwa risasi

Bobi Wine
Spread the love

GARI la Robert Kyagulanyi ‘Bob Wine,’ mgombea urais nchini Uganda kupitia chama cha upinzani cha FDC, limeshambuliwa kwa risasi. Vinaripoti vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea).

Hatua hiyo imesababisha Bobi Wine kusitisha kampeni zake huku maofisa wake kadhaa wakipigwa na kujeruhiwa nchini humo.

Akizungumzia tukio hilo lililotokea Kayunga, mashariki mwa Kampala, Bobi Wine amesema, risasi zilielekezwa kwenye gari lake ambapo zilitoboa matairi ya gari.

Katika sakata hilo, maofisa wanne wa Bobi Wine wamejeruhiwa huku video zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mlipuko uliotokea umbali mchache toka pale alipokuwa.

Takriban wiki mbili zilizopita, watu 54 waliuawa wakati wafuasi wa mgombea huyo walipoandamana kudai aachiliwe huru baada ya kukamatwa na polisi katika mkutano wa kampeni.

Baadaye alishitakiwa kwa kukiuka masharti ya kukabiliana na janga la corona kwa kukusanya umati wa watu, lakini aliachiliwa kwa dhamana. Uchaguzi Mkuu nchini humo unatarajiwa kufanyika Januari 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!