GARI la Robert Kyagulanyi ‘Bob Wine,’ mgombea urais nchini Uganda kupitia chama cha upinzani cha FDC, limeshambuliwa kwa risasi. Vinaripoti vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea).
Hatua hiyo imesababisha Bobi Wine kusitisha kampeni zake huku maofisa wake kadhaa wakipigwa na kujeruhiwa nchini humo.
Akizungumzia tukio hilo lililotokea Kayunga, mashariki mwa Kampala, Bobi Wine amesema, risasi zilielekezwa kwenye gari lake ambapo zilitoboa matairi ya gari.
Katika sakata hilo, maofisa wanne wa Bobi Wine wamejeruhiwa huku video zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mlipuko uliotokea umbali mchache toka pale alipokuwa.
Takriban wiki mbili zilizopita, watu 54 waliuawa wakati wafuasi wa mgombea huyo walipoandamana kudai aachiliwe huru baada ya kukamatwa na polisi katika mkutano wa kampeni.
Baadaye alishitakiwa kwa kukiuka masharti ya kukabiliana na janga la corona kwa kukusanya umati wa watu, lakini aliachiliwa kwa dhamana. Uchaguzi Mkuu nchini humo unatarajiwa kufanyika Januari 2021.
Leave a comment