Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Gari la Bobi Wine lashambuliwa kwa risasi
Kimataifa

Gari la Bobi Wine lashambuliwa kwa risasi

Bobi Wine
Spread the love

GARI la Robert Kyagulanyi ‘Bob Wine,’ mgombea urais nchini Uganda kupitia chama cha upinzani cha FDC, limeshambuliwa kwa risasi. Vinaripoti vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea).

Hatua hiyo imesababisha Bobi Wine kusitisha kampeni zake huku maofisa wake kadhaa wakipigwa na kujeruhiwa nchini humo.

Akizungumzia tukio hilo lililotokea Kayunga, mashariki mwa Kampala, Bobi Wine amesema, risasi zilielekezwa kwenye gari lake ambapo zilitoboa matairi ya gari.

Katika sakata hilo, maofisa wanne wa Bobi Wine wamejeruhiwa huku video zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikionesha mlipuko uliotokea umbali mchache toka pale alipokuwa.

Takriban wiki mbili zilizopita, watu 54 waliuawa wakati wafuasi wa mgombea huyo walipoandamana kudai aachiliwe huru baada ya kukamatwa na polisi katika mkutano wa kampeni.

Baadaye alishitakiwa kwa kukiuka masharti ya kukabiliana na janga la corona kwa kukusanya umati wa watu, lakini aliachiliwa kwa dhamana. Uchaguzi Mkuu nchini humo unatarajiwa kufanyika Januari 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

error: Content is protected !!