Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa UN: video ya ngono yasimamisha kazi wawili
Kimataifa

UN: video ya ngono yasimamisha kazi wawili

UN logo
Spread the love

MAOFISA wawili wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), waliokuwa wanaotajwa kufanya ngono kwenye gari la shirika hilo nchini Israel, wamepelekwa likizo ya bila malipo. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Wafanyakazi hao wawili, walipigwa picha ya video wakiwa kwenye gari lenye nembo ya UN katika mji wa Tel Aviv, Mtaa wa Ufukweni wakiwa wanafanya kitendo hicho.

Kwenye video hiyo iliyowekwa mtandaoni na kuripotiwa pakubwa duniani, mwanamke aliyekuwa amevaa gauni jekundu, alimkalia mwanamue nyuma ya dereva huku wakifanya kitendo hicho.

Mtu mmoja mtaani hapo, akiwa kwa juu kidogo alifanikiwa kupiga picha hiyo. Alifanikiwa kufanya hivyo wakati gari hilo likiwa kwenye taa za barabarani likisubiri kuondoka.

Sekunde chache baadaye, taa ziliruhusu kuondoka na gari hilo liliondoka huku ‘shughuli’ ikiwa inaendelea nyuma ya kiti cha dereva,

Ilikuwa rahisi kuonekana kwa watu hao wakifanya ‘mambo’ kwa kuwa, gari hilo vioo vyake havikuwekwa giza ‘tinted.’

Stéphane Dujarric, Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja UN alitaja kitendo hicho kwamba ni cha kuchukiza na kushtua.

Mpaka sasa, UN imebaini kuwa wanahusika hao ni waajiriwa katika taasisi yake ya Kusimamia Kusitishwa kwa Mapigano (UNTSO).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!