Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rushwa ya ngono Vyuo Vikuu, wanafunzi waonywa
Habari Mchanganyiko

Rushwa ya ngono Vyuo Vikuu, wanafunzi waonywa

Chuo Kikuu cha RUCU
Spread the love

WANAFUNZI wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati wametahadharishwa, kwamba wasipokuwa makini rushwa ya ngono itawaharibia maisha yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Mweli Kilimali, Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Iringa akizungumza na klabu za wapinga rushwa za vyuo vikuu na vya kati mkoani humo.

Ametoa kauli hiyo kutokana na kuwepo kwa taarifa za kukithiri kwa rushwa ya ngono vyuoni, na kwamba wametakiwa kutowafumbia macho walimu na wahadhiri wanaojihusisha na tabia hiyo.

“Nawataka  wanafunzi kuacha tabia ya uvivu wa kujisomea ili mfanye vizuri katika mitihani yenu, mkifanya hivyo mtaepuka kuwashawishi wahadhiri katika rushwa ya ngono au fedha, lakini sio wote wanatoa rushwa ya ngono,” amesema.

Amesema, ubaya wa rushwa ulianzia katika vitabu vya dini ambapo Qur’an Tukufu na Biblia Takatifu, zote zimekema vitendo hivyo vya rushwa vyenye maudhui ya kupora haki.

“Ndugu zangu, rushwa ni adui, rusha ni mbaya, rushwa imekemewa katika vitabu vyetu vitukufu ndani ya Qur’an Tukufu na katika Biblia Takatifu. Rushwa hii ya ngono inavunja utu na kumdhalilisha mtenda na mtendewa, hivyo kataeni rushwa,” amesema.

Profesa Gaudence, Mkuu wa Kitivo cha Elimu katika Chuo Kikuu cha RUCU, alikiri kuwepo kwa vitendo hivyo vyuoni na kuwataka wanafunzi kuacha woga, badala yake watoe taarifa kwa vyombo vinavyoshughulikia masuala ya ukatili wa kijinsia katika ngazi za chuo, polisi au Takukuru.

Martha Magembe, Mshauri wa Wanafunzi wa RUCU amewataka wanafunzi hao kutokuwa chanzo cha rushwa ya ngono, kwa kutoa ushawishi kwa wahadhiri wao.

“Kuna baadhi ya wanafunzi wanafanyiwa vitendo vya kikatili lakini wananyamaza kutokana na woga, au kuhofia kupoteza kitu fulani kutokana na vitisho hivyo, nawaomba mtoe taarifa Takukuru ili tuwabaini wahusika na sheria ichukue mkondo wake,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!