RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua, Mariam Perla Mmbaga kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu (RAS). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kabla ya uteuzi huo, Mariam alikuwa Mkurugenzi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Mariam anachukua nafasi ya Jumanne Sagini.
Mariam ataapishwa Jumatatu tarehe 06 Julai, 2020 saa 4:00 asubuhi Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma.
Leave a comment