Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya ‘Waliokuwa na dereva taxi Arusha, hawajaambukizwa COVID-19’
AfyaHabari Mchanganyiko

‘Waliokuwa na dereva taxi Arusha, hawajaambukizwa COVID-19’

Spread the love

DAKTARI Janeth Mghamba, Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Ufutiliaji wa Magonjwa ya Mlipuko katika Wizara ya Afya amesema, watu 27 waliochukuliwa ili kupimwa kama wana maambukizi ya virusi vya corona jijini Arusha, wapo salama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Amesema, watu walioshukuliwa vipimo ni wale waliobainika kuwa na mawasiliana ama kukutana na dereva wa taksi ambaye alimbeba mgonjwa wa kwanza wa corona nchini.

Mbele ya waandishi wa habari leo tarehe 19 Machi 2020, akiambatana na Dk Faraja Msemwa ambaye ni Mtaalam wa Majanga wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk. Mghamba amesema sampuli za watu hao baada ya kupimwa walibaini kutoadhiriwa na virusi hivyo.

“Hawa walikuwa karibu na dereva na baada ya kuchukuliwa vipimo, wamebainika hawajaambukizwa,” amesema

Amesema, licha ya taarifa hiyo ya kutoathiriwa na virusi hivyo, wataendelea kufuatiliwa mpaka watakapopimwa kwa mara ya tatu kama ambavyo WHO iliagiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!