Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mongella aagiza wanafunzi kushiriki ‘Urithi Festival’
Elimu

Mongella aagiza wanafunzi kushiriki ‘Urithi Festival’

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella
Spread the love

JOHN Mongela, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, amewataka maofisa elimu wa shule za msingi na sekondri mkoani humo, kuwapeleka wanafunzi kushiriki na kujifunza utamaduni wa nchi katika tamasha la Urithi Festival. Anaripoti Charles Mseti, Mwanza … (endelea).

Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya ‘Urithi Wetu Fahali Yetu,’ linatarajiwa kufanyika kitaifa kuanzia tarehe 31 Oktoba hadi 2 Novemba 2019 katika viwanja vya Rock City Mall jijini humo.

Mongella ametoa kauli hiyo leo tarehe 29 Oktoba 2019, alipozungumza na wanahabari kuhusu kilele cha tamasa hilo na kuwa, tamasha hilo lenye lengo la kutambua na kutangaza sanaa na utamaduni wa nchi (Tanzania), litazidi kurudisha uzalendo kwa wananchi.

“Wananchi wote wa mikoa jirani ya Mwanza, wote nina wakaribisha kuja kutambua sanaa na utamaduni wa nchi yetu pamoja na kutangaza sanaa za nchi yetu.

“Niwatake maofisa elimu wa shule zetu za msingi na sekondari, waje na wanafunzi wao katika hili tamasha, kuja kuona utamaduni wetu na sanaa yetu, hii itasaidia kurudisha uzalendo kwa watoto wetu,” amesema Mongella.

Amesema katika tamasha hilo pia kutakuwa na michezo mingine ya mashindano ya baiskeli na mchezo wa bao. hata hivyo Novemba 3 mwaka huu kutakuwa na safari ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Burigi iliyopo  Chato mkoani Geita.

Tamasha hilo limeshirikisha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Wizara ya Maliasili na Utalii na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. Mgeni rasmi katika kilele cha tamasha hilo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!