Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump, Melania watinga Iraq kimyakimya
Kimataifa

Trump, Melania watinga Iraq kimyakimya

Donald Trump
Spread the love

ZIARA ya Rais wa Marekani, Donald Trump na mkewe Melania imefanywa kimyakimya nchini Iraq. Vinaripoti vyombo vya kimataifa … (endelea).

Hata hivyo inaelezwa kuwa, utawala wa Iraq ulikuwa na taarifa ya ujio huo na kuwa, Waziri Mkuu wa Iraq alipanga kukutana naye.

Hata hivyo Trump ameondoka Iraq bila kukutana na mwenyeji wake waziri mkuu Adel Abdul Mahdi kwa madai kuwa, kushindwa kukubaliana jinsi mkutano huo ungefanyika.

Trump na mkewe walisafiri usiku wa Krismasi kwenda nchini humo kuzungumza na wanajeshi wake ambapo aliwaambia Marekani haina mpango ya kuwaondoa kwenye ardhi ya Iraq.

Trump aliwashukuru wanajeshi wake nchini humo kwa kujitolea. Ziara hiyo inafanyika siku chache baada ya waziri wa ulinzi Jim Mattis kujiuzulu kufuatia mgawanyiko wa sera za Trump eneo hilo.

Marekani ina wanajeshi 5,000 nchini Iraq kuunga mkono serikali katika vita dhidi ya kundi la Islamic State.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!