Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Michezo Shabiki apoteza maisha uwanjani
Michezo

Shabiki apoteza maisha uwanjani

Spread the love

SHABIKI wa Inter Milan amepoteza maisha na wengine wanne kujeruhiwa katika mchezo dhidi ya FC Napol uliopigwa kwenye uwanja wa San Siro baada ya kuibuka vurugu kubwa kwa mashabiki wa pande zote mbili kabla ya mechi.

Taarifa kutoka nchini Itaria zinasema kuwa mshabiki huyo alipoteza maisha kwa kugongwa na gari nje ya uwanja kwenye mchezo wa Ligi Kuu uliocheza jana na kushuhudia Inter Milan kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FC Napol.

Katika mchezo huo ambao uligubikwa na vurugu nyingi ndani na nje ya uwanja kiasi cha kupelekea beki wa kati wa klabu ya Napol anaye windwa na Manchester United, Kalidou Koulibaly kutolewa nje ya uwanja baada ya kuoneshewa kadi mbili za njano.

Licha ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa mchezaji huyo, mashabiki wa wa Inter Milan walionekana kufanya vitendo vya ubaguzi wa rangi kwa beki huyo baaada ya kutoa milio kama nyani wakati mchezaji huyo anaposhika mpira uwanjani kiasi kilichompelekea kuandika ujumbe mzito katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.

Vitendo hivyo ambavyo Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kuvipinga vikali lakini bado vinaonekana kushamili kwa wachezaji wenye ngozi nyeusi wanaocheza soka la kulipwa barani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariMichezo

Benki ya NBC yazindua kombe jipya la Ligi Kuu Tanzania Bara

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa Ligi ya NBC , Benki ya Taifa...

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu

Spread the love RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumatatu, tarehe...

error: Content is protected !!