RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli leo tarehe 28 Desemba 2018 atakutana na viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini, watendaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii na mawaziri wa wizara husika, kwa ajili ya kujadili masuala yahusuyo mafao ya wafanyakazi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mapema leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Magufuli pia atazungumza na viongozi hao kuhusu kanuni mpya ya kukokotoa mafao ya wastaafu.
Vyama vitakavyokutana na kuzungumza na Rais Magufuli ikulu jijini Dar es Salaam, ni pamoja na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA), vyama shiriki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSD na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Kanuni mpya ya kikokotoo iliyotolewa hivi karibuni na serikali, ambayo inaelekeza wastaafu kulipwa mkupuo wa asilimia 25 ya mafao pindi watakapostaafu na asimilia 75 inayobaki watakuwa wakilipwa kama pensheni ya kila mwezi.
Baada ya kikokotoo hicho kutangazwa kwa umma, baadhi ya vyama vya wafanyakazi ikiwemo TUCTA, viliipinga kanuni hiyo kwa maelezo kwamba inakandamiza wafanyakazi.
Leave a comment