Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji hospitali za serikali kukaukiwa dawa
Habari za Siasa

Mbunge ahoji hospitali za serikali kukaukiwa dawa

Baadhi ya wananchi wakiwa sehemu ya mapokezi ya hospitali, tayari kwa kupata huduma
Spread the love

MBUNGE wa Siha Dk. Godwin Mollel (Chadema) ameihoji serikali na kutaka ieleze ni kwa nini hospitali zake nyingi   zinakosa dawa muhimu za binadamu wakati katika hospitali binafsi zipo, anaandika Dany Tibason.

Mollel aliuliza swali la nyongeza amesema kumekuwepo na tatizo la hospitali nyingi na vituo vya afya vya serikali kukosa dawa muhimu za binadamu huku dawa hizo zikipatikana katika vituo binafsi au maduka binafsi .

Awali katika swali la msingi la mbunge wa Korogwe mjini,  Mery Chatanda( CCM) alitaka kujua serikali imetoa maelekezo gani pale ambapo Bohari ya Dawa (MSD) wamekuwa hawana baadhi ya dawa zinazohitajika kwa wagonjwa.

“Hospitali za serikali zimeandaliwa kupata huduma za MSD lakini wakati mwingine baadhi ya dawa hazipatikani na hospitali hairuhusiwi kununua dawa nje ya MSD.

“Je serikaki imetoa maelezo gani pale ambapo MSD wamekuwa hawana baadhi ya dawa hizo zinazohitajika na wagonjwa”alisema.

Akijibu maswali hayo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk.Khamis Kigwangwala alisema kuwa kwa sasa hospitali zote pamoja na vituo vya afya vya serikali kuna dawa zaidi ya aina 138 zinazohitajika.

Alisema kuwa kwa sasa dawa nyingi zinapatikana kutokana na kuongezeka kwa pesa katika wizara husika tofauti na ilivyo kuwa hapo hawali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Wanaotaka kujifunza ZEC kwao kukoje?

Spread the loveMKURUGENZI wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Biteko, Nape wanadanganya?

Spread the loveKWA mila na desturi zetu za Kiafrika mkubwa huwa hakosei,...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Miamka 60 ya Muungano: Tunakwama wapi?

Spread the loveRAIS wa Jamhuri, Samia Suluhu Hasssan, Ijumaa iliyopita, aliongoza mamilioni...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

error: Content is protected !!