Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ahoji hospitali za serikali kukaukiwa dawa
Habari za Siasa

Mbunge ahoji hospitali za serikali kukaukiwa dawa

Baadhi ya wananchi wakiwa sehemu ya mapokezi ya hospitali, tayari kwa kupata huduma
Spread the love

MBUNGE wa Siha Dk. Godwin Mollel (Chadema) ameihoji serikali na kutaka ieleze ni kwa nini hospitali zake nyingi   zinakosa dawa muhimu za binadamu wakati katika hospitali binafsi zipo, anaandika Dany Tibason.

Mollel aliuliza swali la nyongeza amesema kumekuwepo na tatizo la hospitali nyingi na vituo vya afya vya serikali kukosa dawa muhimu za binadamu huku dawa hizo zikipatikana katika vituo binafsi au maduka binafsi .

Awali katika swali la msingi la mbunge wa Korogwe mjini,  Mery Chatanda( CCM) alitaka kujua serikali imetoa maelekezo gani pale ambapo Bohari ya Dawa (MSD) wamekuwa hawana baadhi ya dawa zinazohitajika kwa wagonjwa.

“Hospitali za serikali zimeandaliwa kupata huduma za MSD lakini wakati mwingine baadhi ya dawa hazipatikani na hospitali hairuhusiwi kununua dawa nje ya MSD.

“Je serikaki imetoa maelezo gani pale ambapo MSD wamekuwa hawana baadhi ya dawa hizo zinazohitajika na wagonjwa”alisema.

Akijibu maswali hayo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk.Khamis Kigwangwala alisema kuwa kwa sasa hospitali zote pamoja na vituo vya afya vya serikali kuna dawa zaidi ya aina 138 zinazohitajika.

Alisema kuwa kwa sasa dawa nyingi zinapatikana kutokana na kuongezeka kwa pesa katika wizara husika tofauti na ilivyo kuwa hapo hawali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!