Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanaharakati wazidi kumsakama mke wa Mugabe
Kimataifa

Wanaharakati wazidi kumsakama mke wa Mugabe

Mwanamitindo Gabriella Engels aliyeshambuliwa na Grace Mugabe
Spread the love

GABRIELLA Engels, mwanamitindo nchini Afrika Kusini aliyeshambuliwa na Grace Mugabe, mke wa Rais wa Zimbabwe, amepinga kinga ya kidiplomasia inayotolewa na serikali ya nchi yake kwa vigogo, anaandika Irene Emmanuel.

Binti huyo mwenye umri wa miaka 20 anaungwa mkono na kundi la shinikizo, AfriForum, ambalo katika kupinga sheria hiyo wameonyesha ukurasa wa kwanza wa fomu ya maombi kutoka mahakama kuu ya mji mkuu na kudai kwamba waziri wa mambo ya nje, Maite Nkoana Mashabane ameelezea sheria ya kinga ya kidiplomasia vibaya.

AfriForum wamedai kuwa sheria hiyo ya kidiplomasi inayowakinga vigogo na serikali haihusishi vigogo ambao wamesababisha vifo au majeraha kwa wananchi wake.

Polisi wa Afrika Kusini wamesema Grace hajaripoti kituoni kama ambavyo ilikuwa imepangwa na ameondoka nchini na mume wake Robert Mugabe jumapili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!