Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliokufa kwa maporomoko Sierra Leone wazikwa
Kimataifa

Waliokufa kwa maporomoko Sierra Leone wazikwa

Kikosi cha uokoaji kikiendelea kuokoa majeruhi wa Maporomoko ya udongo huko Sierra Leone
Spread the love

NUSU ya maiti 400 zilizotokana na maporomoko ya udongo na mafuriko nje ya mji wa Freetown tayari zimezikwa, anaandika Hamisi Mguta.

Serikali nchini humo ilisema mazishi ya pamoja yangeahirishwa hadi leo ili kutoa fursa kwa ndugu na jamaa kutambua miili ya maiti ya waathirika.

Lakini mkuu wa wataalamu wa magonjwa kutoka mjini Freetown ameliambia shirika la habari la BBC kuwa baadhi ya mazishi yalikuwa yamekwishafanyika.

Imefahamika kuwa mazishi hayo yamehusisha miili ambayo tayari ilitambuliwa au ilikuwa imeharibika kabisa.

Watu wapatao 600 mpaka sasa hawajulikani walipo huku Rais wa Sierra Leone ametangaza siku saba za maombolezi.

Nathaniel Williams ni daktari katika hospitali kuu ya Connaught, iliyopo Freetown, anasema hivi sasa kuna tahadhari kubwa ya kutokea magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu hivyo sasa kunahitajika madawa na vyakula, kwa wale walioathirika.

Hata hivyo, Umoja wa Mataifa nchini humo umesema tayari umeweka mikakati ya kuweza kukabiliana na magonjwa ya milipuko iwapo yatatokea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!