Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanaharakati wahukumiwa kifungo cha maisha nchini Misri
Kimataifa

Wanaharakati wahukumiwa kifungo cha maisha nchini Misri

Moja ya maandamano ya wanaharakati wa Ikhwanul Muslimin
Spread the love

Mahakama ya Jinai nchini Misri imewahukumu kifungo cha maisha jela wanaharakati 43 wa Ikhwanul Muslimin, anaandika Hellen Sisya.

Katika hukumu hiyo mahakama hiyo imesema wanaharakati hao walishiriki maandamano yaliyopigwa marufuku dhidi ya serikali, kuwashambulia maofisa usalama na kupora mali za umma.

Aidha, mahakama hiyo pia imewaamuru watunhao kulipa faini ya Dola za Marekani  948,661 kwa kupora mali za umma.

Wanaharakati wengine tisa wa Ikhwani wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela huku 92 wakiachiwa huru.

Baada ya jeshi la Misri kumuondoa madarakani Muhammad Mursi serikali ilipiga marufuku shughuli zote za kundi hilo la  Ikhwanul Muslimin.

Kadhalika, idadi kubwa ya viongozi na wanachama wa kundi hilo wamefungwa jela na baadhi yao wamehukumiwa adhabu ya kifo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!