Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanaharakati wahukumiwa kifungo cha maisha nchini Misri
Kimataifa

Wanaharakati wahukumiwa kifungo cha maisha nchini Misri

Moja ya maandamano ya wanaharakati wa Ikhwanul Muslimin
Spread the love

Mahakama ya Jinai nchini Misri imewahukumu kifungo cha maisha jela wanaharakati 43 wa Ikhwanul Muslimin, anaandika Hellen Sisya.

Katika hukumu hiyo mahakama hiyo imesema wanaharakati hao walishiriki maandamano yaliyopigwa marufuku dhidi ya serikali, kuwashambulia maofisa usalama na kupora mali za umma.

Aidha, mahakama hiyo pia imewaamuru watunhao kulipa faini ya Dola za Marekani  948,661 kwa kupora mali za umma.

Wanaharakati wengine tisa wa Ikhwani wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela huku 92 wakiachiwa huru.

Baada ya jeshi la Misri kumuondoa madarakani Muhammad Mursi serikali ilipiga marufuku shughuli zote za kundi hilo la  Ikhwanul Muslimin.

Kadhalika, idadi kubwa ya viongozi na wanachama wa kundi hilo wamefungwa jela na baadhi yao wamehukumiwa adhabu ya kifo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!