Wednesday , 15 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba
Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love

MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi ame tumia sherehe za  siku ya Muungano wa Tanganyika kutaja mafanikio ya miaka mitatu ya Rais Dk. Samia Suruhu akisema alitoa Bilioni 124 zilizojenga miradi. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea). 

Amesema serikali ya awamu ya sita inafanya kazi kubwa ya kuwa ondolea wananchi changamoto zinazowakumba hivyo kazi iliyopo ni kuhakikisha miradi inatunza ili iweze kusaidia hadi vizazi vijavyo kwa ni amegusa kila sekta ikiwemo elimu, afya, maji, miundo mbinu na nishati.

DC Kihongosi aliyasema hayo tarehe 26 Aprili, 2024 wakati wa maadhi misho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanzania na Zanzibar yaliyofanyika kijiji na kata ya Kamsamba wilayani Momba mkoani humo.

Amesema kwenye elimu zimetumika, Sh. 31 bilioni, afya Sh. 14.4 bilioni, vifaa tiba Sh. 1.6 bilioni, Maji Sh. 17.8 bilioni huku vitongoji 142 vikiwekewa umeme ambapo vitongoji 153 kazi inaendelea na pia Sh. 6 bilioni zikitumika ujenzi wa barabara, makalavati na madaraja ndani ya miaka mitatu.

Amesema katika kipindi cha mwaka 2021 hadi 2024 cha utawala wake wa miaka mitaatu ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, wilaya ya Momba ilipokea Tsh,124,062,121,574.23 ikiwa ni kiasi cha Tsh, 45,499,583,419.41 zilienda halmashauri ya mji Tunduma na Tsh, 31,870,007,687.56 zilienda halmashauri ya Momba.

Ameongeza kuwa katika sekta ya kilimo mifugo, wameweza kujenga miradi ya kimkakati, soko la kimataifa la mazao na mifugo kakozi,(Maghara ya kuhifadhia mazao), jengo la kuuzia mazao, mnada wa mifugo na jengo la machinjio na pia pikipiki 23 zilinunuliwa kwa ajili ya maafisa kilimo zikiwemo 8 zilizonunuliwa kwa fedha za mapato ya ndani.

Ameongeza kuwa ujenzi wa majosho sita ya kuogeshea mifugo imeje ngwa kwenye vijiji vya Chitete, Msangano, Nzoka, Ivuna, Mkulwe na Mkomba huku ununuzi na usambazaji wa mbegu za ufuta kwa waku lima ukifanyika kuwaongezea tija na hamasa ya stakabadhi ghala ni ikiwemo ununuzi wa chanjo za mifugo.

Ameeleza kuwa Kiasi cha Tsh,1,974,892,771.14 kilitumika kwa ajili ya sensa ya watu na makazi ya 2022 ambapo wilaya ya Momba yenye wakazi 551,090 na kaya 114,687 ambapo halmashauri ya Momba yenye wakazi 259,781 na kaya 58,098 na halmashauri ya Tunduma ina wakazi 291309 na kaya 56,589.

‘’Leo ni kilele cha Muungano ambapo waasisi wa nchi hii mahayati Mwalimu Julias Nyerere na Abed Kalume mwaka 1964 walikubaliana Zanzibar na Tanganyika kuuungana,hivyo kuna kila sababu ya kuimarisha na kuulinda muungano huo na tayari tumeona maendeleo mengi yakifanyika.

Naye Shekhe Mkuu mkoani wa Songwe, Husein Batuza amesema wao kama viongozi wa dini wana kila sababu ya kuliombea Taifa na viongozi wake huku akimsifu Rais Dk. Samia kwa kupeleka fedha nyingi mkoani Songwe zilizojenga miradi ya maendeleo inayogusa jamii.

Diwani mwenyeji Chalambwenge Kakwale, katika maadhimisho hayo mbali na kuipongeza serikali kupeleka fedha nyingi za miradi iliyoje ngwa hata kwenye kata yake,lakini alitumia nafasi hiyo kutoa kero za ukosefu wa X-ray mashine kwenye kituo cha afya Kamsamba ambapo mkuu wa wilaya ameahidi kuifanyia kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia ateua wenyeviti wa taasisi mbalimbali

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amefanya uteuzi wa viongozi...

Habari Mchanganyiko

Afrika Mashariki wasisitizwa ushirikiano kukabiliana na hali mbaya ya hewa

Spread the love  MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaitambulisha rasmi ‘NBC Connect’ Zanzibar

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imetambulisha rasmi huduma yake...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya kidijitali kwa wajasiriamali

Spread the loveBENKI ya NMB imezindua akaunti maalum ya kidijitali iitwayo ‘NMB...

error: Content is protected !!