Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Museveni abadili uongozi wa jeshi
Kimataifa

Museveni abadili uongozi wa jeshi

David Muhoozi (katikati)
Spread the love

YOWERI Museveni, Rais wa Uganda amefanya mabadiliko katika jeshi la nchi hiyo kwa kumteua David Muhoozi kushika nafasi ya Mkuu wa Majeshi (CDF), anaandika Wolfram Mwalongo.

Awali, nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Edward Katumba Wamala ambapo sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Kazi nchini Uganda.

Kabla ya Muhoozi kuteuliwa katika nafasi ya CDF, alikuwa kiongozi mkuu wa jeshi la ardhi la nchi hiyo.

Katika mabadiliko hayo, Rais Museveni amemteua mtoto wake Muhoozi Kainerugaba kuwa mshauri mwandamizi wa masuala ya oparesheni maalum. Kabla ya mtoto huyo kutwaa nafasi hiyo, alikuwa mkuu wa kikosi maalumu (SDF).

SDF ni kitengo cha juu kinachomshauri rais hususani katika masuala ya kiulinzi pamoja na mambo nyeti ya taifa.

Aidha, amemteua Wilson Mbadi, aliyekuwa Mkuu wa Utumishi na Mlinzi wa rais huyo (bodyguard) kwa muda mrefu kuwa msaidizi wa CDF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!