Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Museveni abadili uongozi wa jeshi
Kimataifa

Museveni abadili uongozi wa jeshi

David Muhoozi (katikati)
Spread the love

YOWERI Museveni, Rais wa Uganda amefanya mabadiliko katika jeshi la nchi hiyo kwa kumteua David Muhoozi kushika nafasi ya Mkuu wa Majeshi (CDF), anaandika Wolfram Mwalongo.

Awali, nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Edward Katumba Wamala ambapo sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Kazi nchini Uganda.

Kabla ya Muhoozi kuteuliwa katika nafasi ya CDF, alikuwa kiongozi mkuu wa jeshi la ardhi la nchi hiyo.

Katika mabadiliko hayo, Rais Museveni amemteua mtoto wake Muhoozi Kainerugaba kuwa mshauri mwandamizi wa masuala ya oparesheni maalum. Kabla ya mtoto huyo kutwaa nafasi hiyo, alikuwa mkuu wa kikosi maalumu (SDF).

SDF ni kitengo cha juu kinachomshauri rais hususani katika masuala ya kiulinzi pamoja na mambo nyeti ya taifa.

Aidha, amemteua Wilson Mbadi, aliyekuwa Mkuu wa Utumishi na Mlinzi wa rais huyo (bodyguard) kwa muda mrefu kuwa msaidizi wa CDF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!