Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wastaafu waililia Serikali ya JPM
Habari Mchanganyiko

Wastaafu waililia Serikali ya JPM

Spread the love

ZAIDI ya wastaafu 300 kutoka wilaya za Nyamagana na Ilemela Mkoani Mwanza, wameilalamikia Serikali kwa kuwakata makato makubwa ya pensheni zao za kila miezi mitatu kwani hayaendani na hali halisi ya maisha, anaandika Moses Mseti.

Wakizungumza leo katika zoezi la kufanyiwa uhakiki, linalofanywa na Wizara ya Fedha na Mipango wamedai kwamba licha ya makato hayo makubwa bado pensheni wanayolipwa kwa mwezi haizidi Sh. 80,000/= na 90,000/=

“Kiasi cha fedha tunacholipwa, hakiendani na hali ya maisha ya sasa. Serikali inapaswa kuangalia namna bora ya kutuongezea pensheni za kila mwezi au baada ya miezi mitatu ili kuendana na hali halisi ya maisha,” amesema Salome Sabula, mmoja kati ya wastaafu hao.

Kwa upande wake mstaafu mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Elizabeth Sylvester amesema, “mimi watoto wangu nimesomesha lakini mpaka sasa baada ya Serikali kusitisha ajira wapo tu nyumbai bado naendelea kuwasomesha wengine, sasa Sh. 80, 000/= tunazolipwa kwa mwezi zitasaidia nini?”

Wamesema kipindi walipostaafu mwaka 1990, walilipwa Sh. milioni 4.4 tu huku walimuomba Rais John Magufuli, kuwaangalia wastaafu wa zamani ili waongezewe fedha ili kukabiliana na makali ya maisha.

Stanslaus Mpembe, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha na Mipango amesema lengo la uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na wizara hiyo kwenye mikoa mitano ya Kanda ya ziwa unalenga kubaini wastaafu sahihi wanaopaswa kulipwa na serikali.

“Pamoja na kuhakiki wastaafu hao pia tunalenga kuondoa malalamiko na changamoto za wastaafu zilizokuwepo kwa muda mrefu na tunawahimiza wajitokeza kuhakikiwa kabla ya zoezi hilo kukamilika mnamo tarehe 13 Januari mwaka huu,” amesema Mpembe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!