Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa WHO yaonya mlipuko homa ya Dengue
Kimataifa

WHO yaonya mlipuko homa ya Dengue

Spread the love

 

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limewataka wanachama wake kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya Dengue, unaodaiwa kusababishwa na ongezeko la joto duniani linalochochea ongezeko la mbu wanaosambaza virusi vyake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Tahadhari hiyo imetolewa na mtaalamu wa magonjwa ya kuambukiza kutoka WHO, Jeremy Farrar, aliyetoa wito kwa mataifa kuanzisha mijadala ya kuweka mikakati ya kukabiliana na janga hilo.

Farrar amesema nchi zitakazoathirika na janga hilo katika muongo huu ni za kutoka Amerika ya Kusini, Ulaya Kaskazini na nchi zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara, hususan katika miji yenye watu wengi.

“Tunahitaji kuzungumza zaidi kuhusu Dengue, tunahitaji kuandaa nchi juu ya namna zitakavyokabiliana na mlipuko unaokuja katika siku zijazo kwenye miji mingi mikubwa,” amesema Farrar.

Ugonjwa huo ulioathiri zaidi nchi za Asia na Amerika ya Kusini, unasababisha vifo takribani 20,000 kila mwaka, huku visa milioni 4.2 vikiripotiwa na mataifa mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!