SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limewataka wanachama wake kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya Dengue, unaodaiwa kusababishwa na ongezeko la joto duniani linalochochea ongezeko la mbu wanaosambaza virusi vyake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Tahadhari hiyo imetolewa na mtaalamu wa magonjwa ya kuambukiza kutoka WHO, Jeremy Farrar, aliyetoa wito kwa mataifa kuanzisha mijadala ya kuweka mikakati ya kukabiliana na janga hilo.
Farrar amesema nchi zitakazoathirika na janga hilo katika muongo huu ni za kutoka Amerika ya Kusini, Ulaya Kaskazini na nchi zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara, hususan katika miji yenye watu wengi.
“Tunahitaji kuzungumza zaidi kuhusu Dengue, tunahitaji kuandaa nchi juu ya namna zitakavyokabiliana na mlipuko unaokuja katika siku zijazo kwenye miji mingi mikubwa,” amesema Farrar.
Ugonjwa huo ulioathiri zaidi nchi za Asia na Amerika ya Kusini, unasababisha vifo takribani 20,000 kila mwaka, huku visa milioni 4.2 vikiripotiwa na mataifa mbalimbali.
Leave a comment