NAIBU Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amewataka wakuu wa wilaya nchini kutoka elimu kwa wananchi ngazi ya vijiji,kataka na, Tarafa ikiwemo jamii ya wafugaji kulinda alama za barabarani na miundombinu iliyopo ili kuhepuka uharibifu na ajali zisizokuwa za lazima. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea).
Mhandisi Kasekenya ameyasema hayo leo tare he 6 Oktoba,2023 wakati akikagua barabara yenye urefu wa mita 400 iliyojengwa makao makuu ya wilaya ya Songwe (Mkwajuni) iliyojengwa na wakala wa barabara nchini (TANROADS) mkoani Songwe kwa gharama ya Tsh, Milioni 320.
Amesema wakuu wa wilaya watasaidia kuhepusha ajali endapo watatoa elimu kuanzia ngazi za vitongoji hadi Tarafa wakiwemo wafugaji wenye tabia ya kupitisha kifugo barabarani na kuharibu miundombinu.
Amesema miundombinu ya barabara ni muhimu kwa madereva kwani zinaonesha maeneo hatarishi na hata wapita kwa miguu wanakuwa na uhakika wa usalama wao pindi wanapovuka upande wa pili kwa kuangalia alama zilizopo.
Akizungumzia suala hilo, mkuu wa wilaya ya Songwe Solomon Itunda,amesema ameyapokea maagizo hayo huku akisisitiza kuwa waharibifu wa miundombinu ni sawa na wahujumu uchumi hivyo atahakikisha anatoa elimu kwa jamii na kuchukua hatua za kisheria kwa watakaobainika kuharibu miundombinu.
Aidha Itunda amemshukuru Rais Dr, Samia Suruhu kwa kuleta suruhu kwenye wilaya ya Songwe kwa kuwapatia fedha Bilion 1.3 zinazotumika kujenga miundombinu ya barabara na madaraja fedha zilizotendewa haki na Tanroads, kazi iliyopo ni kuhakikisha miundombinu haiharibiwi.
Leave a comment