WAZIRI Mkuu wa Sri Lanka, Ranil Wickremesinghe ameteuliwa kuwa Rais wa muda baada ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Gotabaya Rajapaksa kukimbilia nchi jirani ya Maldives. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea)
Taarifa iliyotolewa na Spika wa taifa hilo lililopo kusini mwa Asia, imesema Rais Rajapaksa alimfahamisha kuhusu uteuzi huo chini ya Kifungu cha 37.1 cha katiba ya Sri Lanka.
Hata hivyo, hakuna kauli ya moja kwa moja kutoka kwa Rajapaksa mwenyewe.
Kwa mujibu wa Katiba ya Sri Lanka, nafasi ya rais ikiwa wazi, waziri mkuu ataapishwa na kukaimu kwa muda mpaka atakapochaguliwa rais kutoka miongoni mwa wabunge.
Uchaguzi huo unapaswa kufanyika ndani ya siku 30 baada ya Rais kujiuzulu. Spika wa bunge la Sri Lanka alisema uchaguzi unaweza kufanyika tarehe 20 Julai, 2022.
Wakati leo ikiwa ndiyo siku aliyopaswa kutangaza kujiuzulu, imeelezwa kuwa Rais Rajapaksa (73) ameikimbia nchi hiyo kwa ndege ya kijeshi, huku kukiwa na maandamano makubwa yaliyotokana na mzozo wa kiuchumi.
Leave a comment