Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa ugumu wa maisha, Uganda waandamana
KimataifaTangulizi

Kisa ugumu wa maisha, Uganda waandamana

Spread the love

Polisi Uganda imewakamata waandamanaji 12 waliokuwa wakipinga kupanda kwa gharama ya maisha katika eneo la Jinja, lililopo kusini-mashariki mwa nchi hiyo. Inaripoti Mitandao ya kimataifa… (endelea)

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Polisi nchini humo jana tarehe 12 Julai, 2022, James Mumbi imesema viongozi wanane kati ya hao 12 pia walikamatwa na watafunguliwa mashtaka ya kuchochea ghasia nchini humo.

Waandamanaji hao, wanadaiwa kuchoma matairi na kufunga barabara yenye shughuli nyingi mjini Jinja na kuwalazimu madereva wa magari kuungana nao kutaka serikali iwape ruzuku ya chakula cha msingi.

Kwa mujibu wa takwimu rasmi karibuni, kiwango cha mfumuko wa bei kwa bidhaa za chakula kimefikia asilimia 13.1 kwa mwezi Mei 2022.

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu 1986, amewataka raia wake kuishi kwa mpangilio badala ya kupunguza ushuru na kuongeza misaada ya serikali kwa watu walio hatarini zaidi, kama wengi wanavyotaka.

Juni 2022, mwanasiasa wa upinzani na aliyekuwa mgombea urais, Kizza Besigye alifungwa jela na kushtakiwa kwa kuchochea ghasia kwa mara ya pili ndani ya mwezi mmoja, baada ya kuongoza maandamano kadhaa kupinga kupanda kwa gharama ya maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!