Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Sri Lanka akubali kujizulu
Kimataifa

Waziri Mkuu Sri Lanka akubali kujizulu

Spread the love

 

Waziri Mkuu wa Sri Lanka, Ranil Wickremesinghe amekubali kujiuzulu baada ya viongozi wa vyama vya siasa nchini humo kumtaka yeye na rais aliye madarakani kukaa kando. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea). 

Hatua hiyo imetokana na shinikizo la waandamanaji ambao wameyavamia makazi yake na kuyachoma moto kutokana na kughadhibishwa na mdororo wa kiuchumi.

Msemaji wa waziri mkuu, Dinouk Colambage, amesema Wickremesinghe amewaambia viongozi wa chama kwamba atajiuzulu pale ambapo pande zote zitakapokubaliana katika namna ya uundwaji wa serikali mpya.

Ametoa uamuzi huo leo tarehe 9 Julai, 2022 baada ya kufanyika kwa maandamano makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Sri Lanka.

Maelfu ya watu walivunja vizuizi na kuingia kwenye makazi ya Rais Gotabaya Rajapaksa na ofisi iliyo karibu kwa kuonesha hasira zao kwa kiongozi huyo.

Picha za video ziliwaonesha mamia ya waandamanaji wakiwa katika bustani yenye bwawa katika makazi hayo na wengine wakiwa na nyuso za furaha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!