RAIS Sri Lanka, Gotabaya Rajapaksa leo tarehe 9 Julai, 2022 ameripotiwa kuhamishwa na kupelekwa mahali salama baada ya makundi ya watu kuvunja kizuizi kilichokuwa kimewekwa na maofisa wa polisi na kuingia ikulu ya nchi hiyo. Amaripoti Mwandishi Wetu … (emdelea).
Hatua hiyo imekuja baada ya kuibuka kwa maandamano makubwa ambayo yamesababishwa na mdororo wa uchumi tangu nchi hiyo ya Kusini mwa Bara la Asia ipate uhuru huku ikikumbwa na uhaba mkubwa wa mafuta na madawa.
Makumi kwa maelfu ya waandamanaji wanaomtaka Rais Rajapaksa na serikali yake wajiuzulu wamevamia makaazi yake rasmi leo Jumamosi na kuingia Ikulu kisha kuanza kupiga picha na kuogelea kwenye swimming pool lililopo katika jumba hilo.
Rajapaksa amepelekwa mahali salama, amesema Ofisa mmoja katika ofisi yake alipokuwa akizungumza na shirika la habari la DPA.
Leave a comment