Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wananchi wavamia ‘swimming pool’ Ikulu, Rais akimbia
Kimataifa

Wananchi wavamia ‘swimming pool’ Ikulu, Rais akimbia

Spread the love

 

RAIS Sri Lanka, Gotabaya Rajapaksa leo tarehe 9 Julai, 2022 ameripotiwa kuhamishwa na kupelekwa mahali salama baada ya makundi ya watu kuvunja kizuizi kilichokuwa kimewekwa na maofisa wa polisi na kuingia ikulu ya nchi hiyo. Amaripoti Mwandishi Wetu … (emdelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya kuibuka kwa maandamano makubwa ambayo yamesababishwa na mdororo wa uchumi tangu nchi hiyo ya Kusini mwa Bara la Asia ipate uhuru huku ikikumbwa na uhaba mkubwa wa mafuta na madawa.

Makumi kwa maelfu ya waandamanaji wanaomtaka Rais Rajapaksa na serikali yake wajiuzulu wamevamia makaazi yake rasmi leo Jumamosi na kuingia Ikulu kisha kuanza kupiga picha na kuogelea kwenye swimming pool lililopo katika jumba hilo.

Rajapaksa amepelekwa mahali salama, amesema Ofisa mmoja katika ofisi yake alipokuwa akizungumza na shirika la habari la DPA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!