RAIS Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa huzuni taarifa ya kifo cha muigizaji mkongwe Chuma Selemani (Bi Hindu). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (emdelea).
Rais ameyasema hayo leo tarehe 9 Julai, 2022 kupitia taarifa fupi aliyoitoa katika mtandao wa Twitter huku akitoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huo.
“Nimepokea kwa huzuni kubwa taarifa za kifo cha msanii maarufu wa Kaole, Chuma Selemani maarufu ‘Bi Hindu’.
“Uweledi wake wa uigizaji na matumizi ya lugha ya Kiswahili yalileta mvuto kwa watazamaji wa Rika zote. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi. Amin,” amesema Rais Samia.
https://youtu.be/Y060_sjaxWM
Kwa mujibu wa taarifa iliyothibitishwa awali na mwanaye alisema kuwa, mama yake alifariki akiwa nyumbani kwake Magomeni katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Alisema, Bi Hindu alikuwa akisumbuliwa na saratani ya mapafu kwa muda mrefu hadi umauti ulipomkuta. Mwenyenzi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema.
Leave a comment