SHIRIKA la kimataifa la hisani la Save the Children limesema takriban watoto 500 wamefariki kutokana na njaa nchini Sudan. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Shirika hilo kati ya watoto hao 500 pia wapo watoto zaidi ya 20 katika kituo cha watoto yatima kinachosimamiwa na serikali katika mji mkuu Khartoum, tangu mapigano yalipozuka nchini humo mwezi Aprili mwaka huu.
Shirika la Save the Children pia lilisema kuwa karibu watoto 31,000 wanakosa huduma ya lishe na matibabu ya utapiamlo tangu shirika hilo la misaada kusitisha shughuli zake kwenye vituo 57 vya lishe nchini Sudan.
Mzozo huo wa Sudan umegeuza jiji la Khartoum na maeneo mengine ya mijini kuwa viwanja vya vita. Wakazi wengi wanaishi bila maji na umeme, na mfumo wa huduma za afya nchini humo umeporomoka.
Mkurugenzi wa shirika la Save the Children nchini Sudan, Arif Noor amesema hawakutegemea kuwaona idadi kubwa ya watoto kama hao wakifa kwa njaa.
Noor amesema mbali na watoto hao kufa njaa idadi ya watoto walioachishwa shule nchini humo pia imeongeza.
Leave a comment