MWANASIASA mkongwe nchini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira amesema itakuwa ni aibu kwa Serikali iwapo itashindwa kuchukua hatua ya kuboresha ufanisi katika bandari ya Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Akizungumza leo tarehe 29 Julai 2023 katika viwanja vya Kawe jijini Dar es Salaam Wasira amesema wanazungumzia zaidi uwekezaji katika bandari ya Dar es Salaam kwa sababu imekuwa na ufanisi mdogo.
“Bandari ya Dar es Salaam inahudumia tani milioni 18 kwa mwaka, reli ya kati ikikamilika itakuwa na uhitaji tani milioni 25, reli ya Tazara ikiboreshwa pia itabeba tani milioni tano kwa mwaka. Jumla ni tani milioni 30 kwa mwaka lakini bandari hii nahudumia milioni 18 chini ya nusu ya mahitaji,” amesema Wasira.
Leave a comment