OMBWE la kisiasa nchini Sri-Lanka limeendelea kuivuruga nchi hiyo kwa siku ya pili mfululizo baada ya viongozi wa upinzani kushindwa kukubaliana nani atachukua nafasi zilizoachwa na viongozi waliokataliwa na wananchi. Inaripoti mitandao ya kimataifa… (endelea)
Hayo yanajiri wakati waandamanaji nchini humo wanaendelea kukaa katika makazi na ofisi ya Rais Gotabaya Rajapaksa na ya waziri mkuu tangu tarehe 9 Julai, 2022 wakishinikiza viongozi hao waondoke madarakani na wameapa kuendelea kubakia hadi pale viongozi hao watakapojiuzulu rasmi.
Waziri mkuu wa nchi hiyo ya iliyopo kusini mwa Asia, Ranil Wickremesinghe alisema ataachia ngazi pale serikali mpya itakapochaguliwa na saa chache baadae spika wa bunge alitangaza kwamba Rais Rajapaksa atajiuzulu Jumatano.
Viongozi wa upinzani wamekuwa katika mazungumzo ya kuunda serikali mbadala itakayojumuisha vyama vyote na kiongozi mkuu wa upinzani Sajith Premadasa amependekezwa kuwa rais huku Dulla Allahperuma aliyekuwa waziri chini ya Rajapaksa, akipendekezwa kuwa waziri mkuu.
Viongozi hao wameaombwa kujadili watakavyogawana nafasi hizo kabla ya kukutana na spika wa bunge leo jioni.
Aidha, mamilioni ya fedha za rupee yaliyoachwa na rais Gotabaya Rajapaksa nyumbani kwake baada ya kukimbia yatakabidhiwa mahakama hii leo Jumatatu.
Leave a comment