Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wapinzani Sri Lanka ‘washikana uchawi’
Kimataifa

Wapinzani Sri Lanka ‘washikana uchawi’

Spread the love

OMBWE la kisiasa nchini Sri-Lanka limeendelea kuivuruga nchi hiyo kwa siku ya pili mfululizo baada ya viongozi wa upinzani kushindwa kukubaliana nani atachukua nafasi zilizoachwa na viongozi waliokataliwa na wananchi. Inaripoti mitandao ya kimataifa… (endelea)

Hayo yanajiri wakati waandamanaji nchini humo wanaendelea kukaa katika makazi na ofisi ya Rais Gotabaya Rajapaksa na ya waziri mkuu tangu tarehe 9 Julai, 2022 wakishinikiza viongozi hao waondoke madarakani na wameapa kuendelea kubakia hadi pale viongozi hao watakapojiuzulu rasmi.

Waziri mkuu  wa nchi hiyo ya iliyopo kusini mwa Asia, Ranil Wickremesinghe alisema ataachia ngazi pale serikali mpya itakapochaguliwa na saa chache baadae spika wa bunge alitangaza kwamba Rais Rajapaksa atajiuzulu Jumatano.

Viongozi wa upinzani wamekuwa katika mazungumzo ya kuunda serikali mbadala itakayojumuisha vyama vyote na kiongozi mkuu wa upinzani Sajith Premadasa amependekezwa kuwa rais huku Dulla Allahperuma aliyekuwa waziri chini ya Rajapaksa, akipendekezwa kuwa waziri mkuu.

Viongozi hao wameaombwa kujadili watakavyogawana nafasi hizo kabla ya kukutana na spika wa bunge leo jioni.

Aidha, mamilioni ya fedha za rupee yaliyoachwa na rais Gotabaya Rajapaksa nyumbani kwake baada ya kukimbia yatakabidhiwa mahakama hii leo Jumatatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!