RAIA wanne wameuwawa Ukraine na wengine kadhaa , kujeruhiwa baada ya shambulio la Urusi kupiga kituo cha matibabu huko Khirkiv, Polisi wa eneo hilo wameripoti. Inaripoti BBC … (endelea).
Kharkiv ni jiji la pili kwa ukubwa nchini Ukraine , na liko karibu na mpaka wa Urusi upande wa Mashariki.
Leo Ijumaa asubuhi tarehe 25 machi 2022 , kulifuatia mashambuli ya mabomu kwenye miundombinu ya kiraia ambapo raia saba wamejeruhiwa na wengine wanne kufariki.
Mashambulizi hayo yalilenga kituo cha matibabu katika wilaya ya Osnovyansky ya jiji hilo.
BBC bado haijathibitisha taarifa hiyo .Vikosi vya Urusi vimekuwa vikijaribu kuizingira Kharkiv bila mafanikio.
Mwandishi wa BBC Quentin Sommervile, amesema kuwa upinzani wa Ukraine katika mji huo , umekatisha tamaa Warusi ambao wamegeukia mashambuluzi ya mizinga na kuharibu vitongoji vyote .
Leave a comment