Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wananchi DRC kuamua hatima yao leo
Kimataifa

Wananchi DRC kuamua hatima yao leo

Spread the love

NCHI ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), leo tarehe 20 Disemba 2023, inafanya uchaguzi wake mkuu huku vigogo watatu, Rais anayemaliza muda wake ambaye pia ni mgombea wa Chama cha UDPS, Felix Tshisekedi, Moise Katumbi (Ensemble) na Martin Fayulu (ECiDe), wakichuana vikali. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Watu takribani milioni 44 wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo, ambapo vyama vya siasa 19 vimesimamisha wagombea wake kwenye kinyang’anyiro cha urais.

Mbali na uchaguzi wa rais, wananchi watachagua wabunge na wajumbe wa mabaraza ya wilaya.

Matokeo ya uchaguzi huo yataamua hatma ya mamlaka ya Rais Tshisekedi, aliyeingia madarakani tangu 2018, akichukua mikoba ya Joseph Kabila.

Katika kampeni zake, Rais Tshisekedi anawaomba wacongo wamchague kwa muhula wa pili ili aimarishe usalama wa nchi hiyo kwa kudhibiti makundi ya waasi ikiwemo M23, linalosumbua katika Jimbo la Kivu, lililoko Kaskazini mwa Congo.

Tume ya uchaguzi nchini humo imewaahidi waangalizi wa kimataifa kwamba uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki, huku mamlaka zikisema mitandao haitafungwa wakati zoezi hilo likiendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!