Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya
Kimataifa

Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya

Spread the love

Rais wa Kenya, William Ruto amesema serikali ya Ukraine inapanga kuweka kituo cha nafaka mjini Mombasa kama sehemu ya hatua kubwa ya kukabiliana na uhaba wa chakula nchini Kenya na maeneo mengine ya Afrika Mashariki. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea)

Ruto ambaye alikutana na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy pembezoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York nchini Marekani jana Jumanne alisisitiza uungaji mkono wake wa suluhu la amani kwa mzozo wa Russia na Ukraine.

“Huko New York, Marekani nilifanya mazungumzo na Rais wa Zelensky ambaye aliazimia kuanzisha kituo cha nafaka katika Bandari ya Mombasa ili kukabiliana na uhaba wa chakula Afrika Mashariki,” Ruto alisema.

“Kenya inatetea utatuzi wa amani wa mzozo wa Urusi na Ukraine ili kurejesha utulivu, kupunguza mateso ya watu na kukomesha uharibifu wa mali,” aliongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the loveWaziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya...

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

error: Content is protected !!