Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya
Kimataifa

Ukraine kufungua kituo cha nafaka Kenya

Spread the love

Rais wa Kenya, William Ruto amesema serikali ya Ukraine inapanga kuweka kituo cha nafaka mjini Mombasa kama sehemu ya hatua kubwa ya kukabiliana na uhaba wa chakula nchini Kenya na maeneo mengine ya Afrika Mashariki. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea)

Ruto ambaye alikutana na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy pembezoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York nchini Marekani jana Jumanne alisisitiza uungaji mkono wake wa suluhu la amani kwa mzozo wa Russia na Ukraine.

“Huko New York, Marekani nilifanya mazungumzo na Rais wa Zelensky ambaye aliazimia kuanzisha kituo cha nafaka katika Bandari ya Mombasa ili kukabiliana na uhaba wa chakula Afrika Mashariki,” Ruto alisema.

“Kenya inatetea utatuzi wa amani wa mzozo wa Urusi na Ukraine ili kurejesha utulivu, kupunguza mateso ya watu na kukomesha uharibifu wa mali,” aliongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!