MMILIKI wa mtandao wa kijamii X, Elon Mask ambao zamani ulikuwa unaitwa Twitter anatarajiwa kuweka tozo za malipo katika utumiaji wa mtandao huo. Anaripoti Mlelwa Kiwale, TUDARCo kwa msaada wa Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Kwa mujibu wa Mask watumiaji wote wa mtandao X wajiandae kuanza kulipia ili kuweza kupata huduma hizo.
“Tunaelekea kuwa na malipo madogo ya kila mwezi kwa matumizi ya mfumo,” amesema mmiliki wa Tesla na SpaceX.
Musk amekuwa akisema kitu hicho kwa muda mrefu kuwa suluhisho lake la kuondoa roboti na akauti ghushi kwenye jukwaa la mtandao huo ni kutoza ada kwa watumiaji wake ili kuwapa vipengele vyenye machapisho marefu na kuongezeka kwa muonekano wa kipekee katika mtandao huo.
Hata hivyo, katika huduma hizo zilizoboreshwa kwa kulipia kwa mfumo wa X Premium bado kuna watumiaji wanaoweza kutumia mtandao huo bila malipo.
Mpango hho umeungwa mkono Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ambaye alisema mfumo wa malipo ndiyo njia pekee ya kukabiliana na utumizi wa akaunti zinazoendeshwa na roboti.
Leave a comment