Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Jeshi la Polisi laanza uchunguzi wa clip inayosambaa mtandaoni
Habari Mchanganyiko

Jeshi la Polisi laanza uchunguzi wa clip inayosambaa mtandaoni

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime
Spread the love

 

JESHI la Polisi limesema limeona video fupi (clip) ikimwonesha Mtoto aliyefanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Anaripoti Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi, Dodoma … (endelea).

Akitoa taarifa hiyo msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi, SACP David Misime amesema Jeshi hilo limeanza kuifanyia kazi kuanzia ilipoanza kusambaa ili aliyefanya kitendo hicho cha kinyama kisichokubalika aweze kukamatwa na hatua zingine za kisheria ziweze kufuata.

Misime ameongeza kuwa mtoto huyo lazima atakuwa na Mama, Babu, Bibi, Shangazi, Mjomba, Majirani na Viongozi wa Serikali za Mitaa ambapo ameomba ushirikiano wa karibu ili hatua za kisheria kisheria zichukue Mkondo wake.

Msemaji wa Jeshi hilo ametoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za aliyefanya kitendo hicho au mahari kilipo tokea asisite kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi au kwa Kiongozi yeyote yule ili kufanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!