Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sri Lanka bado kwawaka moto, Rais akimbia alikokimbilia
Kimataifa

Sri Lanka bado kwawaka moto, Rais akimbia alikokimbilia

Waandamanaji wakiwa nje ya jengo la Ikulu ya Sri Lanka
Spread the love

RAIS wa Sri Lanka, Gotabaya Rajapaksa leo ameondoka kutoka visiwa vya Maldives alikowasili jana baada ya kuikimbia nchi yake kufuatia shinikizo la maandamano ya umma yanayomtaka kujiuzulu kutokana na mzozo mkubwa wa kiuchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Afisa mmoja wa serikali ya Maldives aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina amesema, Rajapaksa aliondoka katika visiwa hivyo kwa kutumia ndege ya shirika la Saudi Arabia inayoelekea Singapore, ambako anatarajiwa kuishi kwa muda.

Rajapaksa (73) na mkewe waliikimbia Sri Lanka jana Jumatano wakitumia ndege ya jeshi wakati waandamanaji wakiendelea kuyamakata majengo ya serikali kumlazimisha kujiuzulu wakimtwika dhima ya kuwa chanzo cha hali mbaya ya kiuchumi inayoikabili nchi hiyo.

Hata hivyo, inaarifiwa hadi sasa kiongozi huyo hajawasilisha barua yake ya kujiuzulu licha ya kutoa ahadi ya kufanya hivyo jana na badala yake amemteua waziri mkuu, Ranil Wickremesinghe kuwa rais wa muda.

Uteuzi wake, ulitangazwa na Spika wa Bunge, chini ya Kifungu cha 37.1 cha katiba ya Sri Lanka.

Waandamanaji wakiwa ndani ya Ikulu ya Sri Lanka

Kwa mujibu wa Katiba ya Sri Lanka, nafasi ya rais ikiwa wazi, waziri mkuu ataapishwa na kukaimu kwa muda mpaka atakapochaguliwa rais kutoka miongoni mwa wabunge.

Uchaguzi huo unapaswa kufanyika ndani ya siku 30 baada ya Rais kujiuzulu. Spika wa Bunge alisema, uchaguzi unaweza kufanyika 20 Julai 2022.

Mapema jana, afisa wa uhamiaji alisema rais na mke wake, pamoja na walinzi wawili, waliondoka nchini humo kwa ndege ya jeshi, ambayo ilitua katika mji mkuu wa Maldives, Male.

Utorokaji huo wa mapema wa rais unafuatia maandamano makubwa katika taifa hilo, ambalo limekuwa likikabiliana na mzozo mbaya wa kiuchumi, yaliyofikia kilele kwa uvamizi wa makaazi rasmi ya rais na waziri mkuu siku ya Jumamosi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!