Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba waipa pole Yanga kwa ajali ya mashabiki
Michezo

Simba waipa pole Yanga kwa ajali ya mashabiki

Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Simba umetoa pole kwa wapinzani wao Yanga kufuatia ajali ya gari la mashabiki wa timu hiyo lililokuwa linaelekea katika mchezo wao wa leo dhidi ya Coastal Union, jijini Arusha. Anaripoti Urumasalu Kisung’uda, TUDARCo … (endelea).

Ajali hiyo iliyosababisha kifo cha mshabiki mmoja na majeruhi watano ilitokea jana usiku tarehe 19 Agosti, 2022 katika barabara ya Bagamoyo eneo la Mwetemo.

Taarifa iliyotolewa na Uongozi wa Simba imetoa pole kwa ndugu wa marehemu pamoja na kuwaombea mashabiki waliopata majeraha katika ajali hiyo.

https://twitter.com/SimbaSCTanzania/status/1560936973602283521/photo/1

Majeruhi watano wa ajali hiyo, wawili wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kutokana na majeraha makubwa waliyoyapata ilhali wengine watatu wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo baada ya kupata majeraha madogo madogo.

Chanzo cha ajali hiyo ni gari iliyokuwa imebeba mashabiki wa Yanga kutaka kulipita gari lingine lililokuwa mbele yake (overtake) na kukutana na gari hilo la mzigo aina ya Canter ambalo katika harakati za kukwepa kugongana uso kwa uso likaipiga ubavuni (pasi) basi hilo aina ya Coaster.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!