Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Samia awapa ujumbe wanafunzi darasa la saba
Elimu

Rais Samia awapa ujumbe wanafunzi darasa la saba

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amewatakia heri wanafunzi wote wa darasa la saba wanaoanza mitihani yao ya kuhitimu leo Jumatano. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kupitia akaunti yake ya Mtandao X, Rais Samia ameandika; “Mmefikia hatua muhimu ya safari yenu ya awali, kuelekea njia mtakazochagua siku za usoni katika kutoa mchango wenu kusukumu mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa letu.

.”Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu aliyewasimamia toka mwanzo wa safari hii ya elimu hadi sasa, akawape utulivu na afya njema, ili mfanye vizuri mitihani yenu.” ameongeza

Amesma Serikali tayari imekamilisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote mtakaoendelea na kidato cha kwanza mwaka 2024.

Jumla ya watahiniwa milioni 1.3 wa Tanzania Bara wanatarajia kuanza mtihani wa kumaliza elimu ya msingi waliyoianza miaka saba iliyopita huku wakionywa kuepuka udanganyifu. 

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limesema mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi (Primary School Leaving Examination PSLE) itafanyika kwa siku mbili kati ya kuanzia tarehe 13 na 14 Septemba 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!