Rais Samia Suluhu Hassan amewatakia heri wanafunzi wote wa darasa la saba wanaoanza mitihani yao ya kuhitimu leo Jumatano. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kupitia akaunti yake ya Mtandao X, Rais Samia ameandika; “Mmefikia hatua muhimu ya safari yenu ya awali, kuelekea njia mtakazochagua siku za usoni katika kutoa mchango wenu kusukumu mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa letu.
.”Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu aliyewasimamia toka mwanzo wa safari hii ya elimu hadi sasa, akawape utulivu na afya njema, ili mfanye vizuri mitihani yenu.” ameongeza
Amesma Serikali tayari imekamilisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote mtakaoendelea na kidato cha kwanza mwaka 2024.
Jumla ya watahiniwa milioni 1.3 wa Tanzania Bara wanatarajia kuanza mtihani wa kumaliza elimu ya msingi waliyoianza miaka saba iliyopita huku wakionywa kuepuka udanganyifu.
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limesema mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi (Primary School Leaving Examination PSLE) itafanyika kwa siku mbili kati ya kuanzia tarehe 13 na 14 Septemba 2023.
Leave a comment