RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Viongozi hao wameapishwa leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.
Pia, Rais Magufuli ameshuhudia uapisho wa wakuu wa wilaya za Ilala, Maswa, Kalambo, Rombo na Geita.
Soma zaidi:
-
Kafulila na Katambi ‘Out,’ Ma DC, DAS wateuliwa
-
Rais Magufuli abadili uteuzi RC Njombe
-
Rais Magufuli ateua naibu katibu mkuu
-
Rais Magufuli ateua RC, katibu mkuu na DC Dodoma
Walioapishwa ni; Mhandisi Marwa Mwita Bubirya Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe akichukua nafasi ya Christopher Ole Sendeka, Dk. Aloyce Nzuki, kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii na Mhandisi Anthony Sanga, kuwa katibu Mkuu, Wizara ya Maji akichukua nafasi ya Profesa Kitila Mkumbo.
Wengine ni; Dk. Seif Shekilage, kuwa katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kuchukua nafasi ya David Kafulila. Dk. Allan Kijazi, Kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii.
Rais Magufuli amemwapisha Mhandisi Nadhifa Kemikimba, kuwa Naibu katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Dk. Mwinyi Talib Haji, kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Leave a comment