Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kura za maoni CCM: Rais Magufuli awapa maagizo wasimamizi
Habari za SiasaTangulizi

Kura za maoni CCM: Rais Magufuli awapa maagizo wasimamizi

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaosimamia mchakato wa kura za maoni, kutafuta wagombea wa chama hicho nafasi za udiwani, ubunge na uwakilishi kuwa wawazi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam …(endelea).

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020, katika hafla ya uapisho wa viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni iliyofanyikia Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

        Soma zaidi:

Mchakato wa kura za maoni kwa chama hicho unafanyika kwa siku mbili leo na kesho Jumanne.

Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, amesema wanachama 10,367 wa CCM wametia nia kugombea ubunge na uwakilishi nchi nzima ambapo  waliokamilisha taratibu na kuzirejesha ni 10,321.

“Nilikua napata taarifa leo kwa ajili ya kugombe nafasi mbalimbali katika nchi nzima, walikuwa ni 10,367 na katika hao wamekamilisha taratibu na kurudisha fomu ni 10,321, kwa hiyo hawakurudisha 46 katika nchi nzima,” amesema Rais Magufuli.

Mwenyekiti huyo wa  CCM amewataka wasimamizi wa kura za maoni, waendeshe michakato hiyo kwa uwazi bila mizengwe, ili mtia nia anayestahili kupendekezwa kugombea katika uchaguzi huo, apate haki yake.

Rais Magufuli amesema zoezi la kuhesabu kura lifanyike kwa uwazi mbele ya wajumbe, kama ilivyofanyika katika Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), wa kutuea mgombea Urais wa Tanzania na Zanzibar.

Mkutano wa NEC ulifanyika tarehe 10 Julai 2020 jijini Dodoma, ambapo ulimteua Dk. Hussein Mwinyi, kuwa mgombea Urais wa CCM Zanzibar na Rais Magufuli kuwa  mgombea Urais wa Tanzania.

“Matumaini yangu watakaosimamia kura za maoni watasimamia kwa uwazi bila mizengwe yoyote ili kila mwenye haki apate haki yake.”

“Ningetamani viongozi watakaosimamia kwa leo na kesho zikimaliza kupigwa kura, zikafanyike kama ilivyokuwa halmashauri kuu, zihesabiwa hadharani,” amesema Rais Mgufuli.

Rais Magufuli amewapongeza WanaCCM waliotia nia, huku akiwasisitiza wasimamizi wa zoezi hilo, kutenda haki kwa ajili ya kuimarisha umoja wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!