RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk. Mwinyi Talib Haji kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)
Kabla ya uteuzi huo, Dk. Haji alikuwa Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Zanzibar na anachukua nafasi ya Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi.
Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania imesema, uteuzi wa Dk. Haji unaanza leo Jumamosi tarehe 18 Julai, 2020.
Msigwa amesema, Dk. Haji anatakiwa kuwepo Ikulu, Chamwino jijini Dodoma tarehe 20 Julai, 2020 saa 4:00 asubuhi.
Soma zaidi..
Leave a comment