RAIS Putin ametoa onyo kwa wale wanaopinga hatua ya Urusi nchini Ukraine “kutozidisha tatizo kuwa baya zaidi” kwa kuiwekea nchi yake vikwazo zaidi. Inaripoti BBC … (endelea).
Rais wa Urusi alikuwa akizungumza katika mkutano wa serikali uliotangazwa kwenye kituo cha habari cha Rossiya 24 kinachomilikiwa na serikali.
“Hatuna nia mbaya dhidi ya majirani zetu,” Putin amedai.
Na anasema serikali yake haioni ” haja” kwa majirani zake kuchukua hatua zaidi ambazo “zitafanya uhusiano wao kuwa mbaya zaidi”.
“Nadhani kila mtu lazima afikirie jinsi ya kurekebisha uhusiano, kushirikiana kawaida na kukuza uhusiano kama kawaida,” ameongeza.
Haya yanajiri wakati mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi za Magharibi wakikusanyika mjini Brussels kutafakari jinsi ya kuishinikiza Urusi kusitisha vita.
Putin pia anarudia madai yake ya awali kwamba hatua zote zilizochukuliwa na jeshi la Urusi hadi sasa zimefanywa “pekee katika kukabiliana na baadhi ya hatua zisizo za kirafiki dhidi ya Urusi”.
Leave a comment