Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Putin aonya vikwazo zaidi dhidi ya Urusi
Kimataifa

Putin aonya vikwazo zaidi dhidi ya Urusi

Spread the love

 

RAIS Putin ametoa onyo kwa wale wanaopinga hatua ya Urusi nchini Ukraine “kutozidisha tatizo kuwa baya zaidi” kwa kuiwekea nchi yake vikwazo zaidi. Inaripoti BBC … (endelea).

Rais wa Urusi alikuwa akizungumza katika mkutano wa serikali uliotangazwa kwenye kituo cha habari cha Rossiya 24 kinachomilikiwa na serikali.

“Hatuna nia mbaya dhidi ya majirani zetu,” Putin amedai.

Na anasema serikali yake haioni ” haja” kwa majirani zake kuchukua hatua zaidi ambazo “zitafanya uhusiano wao kuwa mbaya zaidi”.

“Nadhani kila mtu lazima afikirie jinsi ya kurekebisha uhusiano, kushirikiana kawaida na kukuza uhusiano kama kawaida,” ameongeza.

Haya yanajiri wakati mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi za Magharibi wakikusanyika mjini Brussels kutafakari jinsi ya kuishinikiza Urusi kusitisha vita.

Putin pia anarudia madai yake ya awali kwamba hatua zote zilizochukuliwa na jeshi la Urusi hadi sasa zimefanywa “pekee katika kukabiliana na baadhi ya hatua zisizo za kirafiki dhidi ya Urusi”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!