KATIBU Mkuu wa Umoja wa Kujihami-NATO, Jens Stoltenberg, amekutana na Katibu Mkuu wa Marekani, Antony Blinken pamoja na mawaziri wa mambo ya nje wa wanachama wa umoja huo Brussels nchini Ubelgiji, kwa lengo la kujadili hatua za kuchukua juu ya uvamizi wa Urusi nchini Ukreini. Inaripoti ABC News … (endelea).
Katika mkutano na waandishi wa habari kabla mkutano huo, Blinken na Stoltenberg alilaani mashambulizi yanayofanywa na Urusi kwa raia wa Ukreini na kutoa maoni juu ya ripoti ya mashambulizi katika mitambo ya nishati ya nyuklia.
“Hii ni ishara tu ya vita ya kizembe na umuhimu wa kuhakikisha inakoma na umuhimu wa Urusi kuondoa vikosi vyao vyote na kuunga mkono juhudi za kumaliza mzozo kwa diplomasia,” Stoltenberg amewaambia waandishi wa habari.
“Tunatoa misaada kwa Ukreini na wakati huo huo NATO si sehemu ya mzozo. NATO ni umoja wa kujihami, hatutafuti mzozo wa kivita na Urusi.”
Blinken alisisitiza kuwa NATO na Marekani “hazitaki mgogoro.”
“Lakini kama mzozo ukija kwetu, tupo tayari,” aliongeza “na tutalinda hata inchi moja ya mipaka yetu.”
Leave a comment