Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ngome ya wanawake ACT-Wazalendo yawakumbuka wazazi waliojifungua
Habari za Siasa

Ngome ya wanawake ACT-Wazalendo yawakumbuka wazazi waliojifungua

Spread the love

 

WANAWAKE wa ACT Tanzania waadhimisha siku ya wanawake Duniani kwa kuwatembelea wazazi katika Kituo cha Afya cha Palestina Sinza jijini Dar es salaam. Anaripoti Rhoda Kanuti, Dar es Salaam … (endelea).

Tukio hilo limefanyika leo Machi 4, 2022, ambapo sambamba na kuwatembelea pia waliwapelekea vitu mbalimbali kama vile sabuni, mafuta ya kupaka na nepi za watoto.

Akizungumza kwaniaba ya wenzake, Katibu Ngome ya Wanawake, Bonafasia Mapunda amesema wamekwenda kuadhimisha siku ya wanawake Duniani ambayo kaulimbiu ya mwaka huu inasema usawa wa kijinsia kwa maendeleo.

“Usawa wa kijinsia uko katika pande nyingi kama vile Uchumi, Kisiasa, na kijamii. Kwenye kijamii ndio tunaanzia kwenye kazi kubwa ya uumbaji hivyo tunahitaji kuwatia moyo wanawake kwasababu kama wameweza kuleta viumbe dunia basi wanaweza kufanya shughuli yoyote ya kijamii na kuleta maendeleo pia wanaweza kuingia kwenye siasa nakuwa viongozi bora,’’ amesema na kuongeza kuwa wameona waende kuwatembelea na kuwapa pongezi kwa kazi kubwa walioifanya yakuwaleta duniani watoto wakiume na wakike.

Mapunda alihitimisha kwa kumshukuru Meneja wa Wazazi kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuwahudumia wanawake wanao leta watoto duniani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!