Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Padre Mrusi akamatwa kwa mahubiri ya kupinga vita
Kimataifa

Padre Mrusi akamatwa kwa mahubiri ya kupinga vita

Spread the love

KUNDI la wanaharakati huko Urusi limeripoti kwamba padre ambaye alitoa mahubiri ya kupinga vita nchini Ukraine Jumapili, amekamatwa na anatarajiwa kufunguliwa mashtaka leo tarehe 7 Machi, 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Mwandishi wa BBC nchini Urusi, Andrey Zakharov ameripoti kuwa padre John Burdin aliwekwa chini ya ulinzi muda mfupi baada ya kutoa mahubiri katika kanisa dogo kwenye kijiji cha Karabanovo.

Padre huyo alihubiri dhidi ya vita akiwaelezea wananchi kile kinachoendelea nchini Ukrenia akiwaonesha picha za matukio ya vita.

Polisi nchini Urusi wamemfungulia mashtaka ya kudharau kazi za jeshi, kosa la jinai ambalo limeanzishwa na Serikali ya Urusi wiki iliyopita.

Tangu kuanza kwa vita nchi Ukrenia kumekuwa na vizuizi vingi kwa wanaharakati nchini Urusi ambapo pamoja na kujua athari bado maelfu ya watu wameendelea kuandamna barabarani katika miji mingi kupinga vita hivyo.

Zaidi ya watu 13,000 wameshakamatwa wakiwemo 4,600 waliokamatwa Jumapili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!